Search This Blog
Sunday, October 20, 2019
Afrika Kusini yazima ndoto za Japan kufikia nusu fainali Kombe la Dunia la Rugby
Afrika Kusini jana ilizima ndoto za Japan za kufikia nusu fainali ya Kombe la Dunia kwa kuibamiza kwa 26-3 katika hatua ya robo fainali huko Tokyo na kujikatia tiketi ya kupambana na wakali Wales katika nusu fainali ya kombe la dunia la raga.
Japan iliitambia Afrika Kusini kwa 34-32 katika kombe la dunia lililopita lakini mechi ya jana iliyochezwa Tokyo ilikuwa zamu yao kulipiza kisasi mabingwa hao mara mbili duniani wa raga.
Afrika Kusini sasa imetinga nusu fainali na itacheza na Wales walioishinda Ufaransa kwa 20-19 mapema jana. Springboks ya Afrika Kusini iliyowahi kushinda Kombe la Webb Ellis mwaka 1995 na 2007, sasa ina ndoto ya kulinyakua kombe la dunia la 2019.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...


No comments:
Post a Comment