Search This Blog

Sunday, September 15, 2019

Tunisia kufanya uchaguzi wa Rais leo

Tunisia inatarajiwa kufanya uchaguzi wa rais leo. Hii itakuwa mara ya pili kwa nchi hiyo kufanya uchaguzi huru wa rais kwa njia ya demokrasia tangu kutokea vuguvugu lililotokea mwaka 2011 na kumuondoa madarakani aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Zine el-Abidine Ben Ali.

Wagombea 26 akiwemo Waziri Mkuu Youssef Chahed watashiriki uchaguzi huo. Hata hivyo haijajulikana wazi ni nani atafaulu kuingia kwenye duru ya pili ya uchaguzi huo.

Wapiga kura milioni saba wanatarajiwa kushiriki uchaguzi huo, baada ya kumalizika rasmi kampeni zilozojikita zaidi kwenye changamoto za kijamii na kiuchumi zinazoizonga nchi hiyo ya Afrika kaskazini.

Hapo jana, wagombea wawili waliamua kujitoa kwenye uchaguzi huo na badala yake kumuunga mkono waziri wa ulinzi Abdelkarim Zbidi.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...