Rais Muhammadu Buhari wa Nigeria anatarajiwa kufanya ziara ya kikazi nchini Afrika Kusini. Kwa mujibu wa ofisi ya rais ya Afrika Kusini ziara hiyo inatokana na vurugu za chuki dhidi ya wageni, ambazo zimesababisha mvutano baina ya mataifa hayo mawili.
Katika siku za hivi karibuni maeneo ya jiji la kibiashara la Afrika Kusini, Johannesburg, yalikumbwa na vurugu zilisosababisha mauwaji dhidi ya wageni, wengi wa walengwa wakiwa wafanyabiashara wa Nigeria na mali zao.
Vurugu hizo zilisababisha mashambulizi ya kulipiza kisasi dhidi ya makupuni ya Afrika Kusini nchini Nigeria na kufungwa kwa muda mfupi kwa ubalozi wa Afrika Kusini mjini Lagos.
Takribani watu 10 walipoteza maisha katika vurugu hizo na mamia ya maduka yaliharibiwa vibaya.
Taarifa ya ofisi ya rais ya Afrika Kusini imesema ziara ya Buhari ina lengo la kuimarisha uhusiano baina ya mataifa hayo mawili na kufanya jitihada ya pamoja katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili watu na biashara kati ya Afrika Kusini na Nigeria.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment