Mfalme Salman wa Saudi Arabia amemuondoa katika wadhfa wake waziri wa nishati na kumpa nafasi hiyo mwanawe, aitwae Mwanamfalme Abdulaziz bin Salman.
Nafasi ya uwaziri wa nishati, ni moja kati vyeo muhimu katika taifa hilo la kifalme. Khalid al-Falih ameondoshwa katika nafasi yake ikiwa ni siku chache baada ya kupoteza nafasi yake kama mwenyekiti wa bodi ya kampuni kubwa ya mafuta ya serikali iitwayo Aramco.
Al-Falih vilevile alishuhudia hadhi yake ikipungua juma lililopita pale ambapo iliundwa wizara mpya ya madini na viwanda, na kuiondoa sekta hiyo kutoka katika uangalizi wa wizara ya nishati.
Waziri mpya wa Nishati Mwanamfalme Abdulaziz na waziri wa zamani wa nchi na masuala ya nishati Mwanamfalme Mohammed bin Salman ni ndugu wa baba mmoja. Inaaminika ndugu hao wawili hawana uhusiano wa karibu.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment