Jeshi la wanamapinduzi wa Iran limeonya kuwa litashambulia kundi lolote litakaloleta uchokozi dhidi ya nchi hiyo.
Taharuki katika eneo hilo la ghuba imeongezeka baada ya mashambulizi dhidi ya viwanda vya mafuta nchini Saudi Arabia mwishoni mwa wiki iliyopita na Marekani na Saudia Arabia zimeilaumu Iran kwa mashambulizi hayo.Iran imekanusha kuhusika.
Katika mkutano na wanahabari ulioonyeshwa kupitia kituo cha habari cha runinga nchini humo, mkuu wa jeshi hilo meja jenerali Hossein Salami ameonya kuwa kiwango chochote cha uchokozi hakitavumiliwa na kwamba wanakadiria adhabu na wataendelea hadi kuharibiwa kabisa kwa kundi lolote la uchokozi.
Salami amesema kuwa Iran haitaki kuanzisha vita lakini akasisistiza kuwa vikosi vyake vimefanya mazoezi ya vita na viko tayari kwa hali yoyote ile.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayeshughulikia Sekta ya Ujenzi, Arch. Elius Mwakalinga, akitoa maelekezo kwa Kai...

No comments:
Post a Comment