Search This Blog
Thursday, August 8, 2019
Umoja wa Ulaya watafuta Dola Milioni 56 kuwasaidia wanaokumbwa na njaa Afrika Mashariki
Umoja wa Ulaya (EU) umesema kwamba unatafuta Dola Milioni 56 kwa ajili ya kusaidia watu wanaokumbwa na njaa katika kanda ya Afrika Mashariki.
Muungano huo umesema kwamba fedha hizo zitatumika kusaidia watu milioni 28 nchini Somalia, watu milioni 22.6 nchini Ethiopia, watu milioni 3 nchini Kenya na watu milioni 2.24 nchini Uganda wote ambao wanakumbwa na kiangazi.
“Katika ziara zangu kwenye nchi za kanda ya Afrika Mashariki nimeshuhudia jinsi mabadiliko ya hali ya hewa yanaathiri wakazi wa eneo hili. Msaada wetu utawezesha waathiriwa kupokea usaidizi wa kibinadamu,” alisema Christos Stylianides- kamishna wa msaada wa kibinadamu na udhibiti wa majanga wa EU.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment