Search This Blog

Thursday, August 8, 2019

Aliyekuwa Rais wa Brazil kuhamishiwa Gereza la Sao Paulo


Mahakama ya juu nchini Brazil imebatilisha uamuzi wa hapo awali wa kumuhamisha aliyekuwa rais wa nchi hiyo Luiz Inacio Lula da Silva kutoka kwenye gereza la muda mfupi la Curitiba anakozuiliwa na kumpeleka katika gereza la umma katika jimbo la Sao Paulo.

Lula amekuwa akizuiliwa katika gereza la Curitiba kwa zaidi ya mwaka moja. Uamuzi wa kuondoa Lula kutoka gereza hilo la Curitiba uliafikiwa juzi asubuhi huku jaji msimamizi akidai kuwepo kwa changamoto za kuweka kiongozi huyo kwenye gereza hilo kwa kuwa lilitengenezwa kuzuilia wafungwa kwa muda mfupi.

Vilevile, jaji huyo alitaja fujo ambazo hutokea kila mara baina ya wafuasi wa Lula na wapinzani wake mbele ya gereza hilo.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...