Search This Blog
Tuesday, August 27, 2019
Serena adhihirisha umwamba wake kwa Sharapova
Bingwa mara nyingi wa tenisi duniani Serena Williams amerudi kivingine na kudhihirisha umwamba wake mbele ya Maria Sharapova katika michuano ya wazi ya tenisi ya Marekani, mchezo uliochezwa uwanja wa Arthur Ashe.
Mambo mengi yamebadilika tangu wacheza tenisi hao wawili walipokutana mara ya mwisho katika michuano hii Januari 2016, huku Sharapova akiendelea kuwa mpinzani halisi wa Serena.
Ushindi wa seti 6-1, 6-1 ulihitaji dakika 59 tu kwa Serena kumshinda Sharapova. Kocha wa Serena, Patrick Mouratoglou amesema ushindi wa Serena, umetokana na kuweka juhudi katika mazoezi na kuyafanyia kazi makosa yaliyojitokeza katika michuano ya mwisho ya tenisi ambapo alishindwa kufua dafu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment