Search This Blog
Tuesday, August 27, 2019
Kiswahili ni kiunganishi kati ya Rwanda na Zanzibar
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameeleza kuwa lugha ya Kiswahili itakuwa ni kiunganishi kizuri katika kukuza ushirikiano na uhusiano kati ya Rwanda na Zanzibar.
Rais Dk. Shein aliyasema hayo Ikulu mjini Zanzibar wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Rwanda nchini Tanzania Eugine Kayihura ambaye alifika Ikulu kwa ajili ya kuaga.
Katika maelezo yake, Rais Dk. Shein alimueleza Balozi Kayihura kuwa azma ya Rwanda na Zanzibar kushirikiana katika sekta ya elimu hasa katika mafunzo ya lugha ya Kiswahili itajenga uhusiano mwema kati ya pande mbili hizo.
Rais Dk. Shein alieleza kuwa hatua hiyo itakuwa na mafanikio makubwa hasa ikizingatiwa kuwa hivi sasa lugha ya Kiswahili tayari imeteuliwa kutumika rasmi katika Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment