Search This Blog

Friday, August 23, 2019

Ndege ya Air Tanzania yakamatwa Afrika Kusini


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isaack Kamwelwe ameomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza kwa abiria wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) waliokuwa wasafiri kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Oliver Tambo jijini Johannesburg Afrika Kusini kuelekea jijini Dar es salaam nchinj Tanzania kufuatia ndege hiyo kushindwa kufanya safari hiyo kama ilivyopangwa.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo serikali imepokea kutoka kwa balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, ndege hiyo imezuiliwa kwa amri ya mahakama ya Gauteng ya jijini Johannesburg.

Aidha, taarifa hiyo ya wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Leonard Chamuriho imesema kuwa serikali kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa inafuatilia suala hilo ili ndege hiyo iachiwe mara moja na kuendelea na safari zake kama kawaida.


No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...