Search This Blog
Friday, August 23, 2019
Moto Waendelea Kuteketeza Msitu Mkubwa wa Amazon
Bolivia imetoa wito wa kuwepo kwa ushirikiano wa nchi tatu, utakaohusisha Brazil na Paraguay, kuzima moto unaoendelea kuteketeza kwa kasi kubwa msitu mkubwa dunani wa Amazon uliopo kati ya nchi hizo tatu.
Maafisa katika mkoa wa Santa Cruz, wanakadiria kwamba moto huo ulioenea maeneo mbali mbali ya mashariki mwa Bolivia, tayari umekwisha teketeza zaidi ya hekta 450,000.
Aidha, Jeshi la Bolivia linaendelea na juhudi za kuzima moto huo ambao umefikia sehemu ya daraja la Rio Negro, kati ya miji ya Puerto Suarez na Puerto Busch, mpakani mwa Brazil, Paraguay na Bolivia.
Hata hivyo, waziri wa ofisi ya Rais wa Bolivia, Huan Ramon Quintana, ametoa wito wa ushirikiano ili waweze kufanikiwa kuuzima moto huo huku moto huo ukitapakaa na kuendelea kuteketeza msitu huo wa Amazon.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment