Mashirika ya ndege ya British Airways la Uingereza na Lufthansa la Ujerumani yamesitisha ghafla safari za kwenda Cairo, nchini Misri kufuatia wasiwasi wa kiusalama, ingawa hayakueleza kwa kina kuhusu wasiwasi huo.
British Airways ndio iliyoanza kwa kusimamisha safari zake kwa siku saba, kuanzia jana Jumamosi, kama tahadhari ili kuruhusu kufanyika tathmini ya kina. Lufthansa pia ilisitisha safari zake za Misri kutokea Munich na Frankfurt, lakini lenyewe likisema lilikuwa linafuatilia hali ilivyo.
Wizara ya mambo ya nje ya Uingereza imesema ndege zinazotoka Misri kwenda Uingereza pia zilipitia hatua za nyongeza za kiusalama, huku ikiwataka abiria kutoa ushirikiano kamili na maafisa wa usalama kwenye viwanja vya ndege.
Maafisa wa Misri walinukuliwa kwa masharti ya kutotajwa majina yao wakisema mashirika mengine ya ndege yalikuwa yakiendelea na safari kama kawaida. Lufthansa nayo baadae ilisema inataraji kurejesha safari zake hii leo.
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment