Search This Blog

Sunday, July 21, 2019

Huenda Iran ikaongezewa vikwazo zaidi na Uingereza

Serikali ya Uingereza inapanga kuiongezea vikwazo Iran, baada ya nchi hiyo kuiteka meli yake ya mafuta katika Ghuba ya Uajemi.

Gazeti la Daily Telegraph la Uingereza limeripoti kwamba Waziri wa Mambo ya Nje Jeremy Hunt huenda baadae hii leo, akatangaza hatua za kidiplomasia na kiuchumi zitakazochukuliwa dhidi ya Iran.

Uingereza, huenda pia ikaomba kurejeshwa upya kwa vikwazo ambavyo awali Iran iliwekewa na Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya. Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Heiko Maas ametahadharisha kwamba mzozo huo kati ya Uingereza na Iran unaweza kuongezeka.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...