Search This Blog
Thursday, June 27, 2019
Mexico: Polisi wanene kufukuzwa kazi
Maafisa wa polisi wanaotaka kujiunga na kikosi kipya cha ulinzi wa taifa nchini Mexico wamepewa hadi miezi sita kupunguza uzani la sivyo wafutwe kazi.
Maafisa hao wamepewa agizo hilo wanapoendelea na shughuli ya kukabiliana na wahamiaji haramu.
Maafisa 625 tayari wamefeli vigezo vya kiafya vya kujiunga na kikosi hicho kitakachohudumu katika mpaka wa Kaskazini na Kusini mwa nchi hiyo kwa miezi sita au zaidi, lilisema gazeti la El Financiero katika ripoti yake.
Maafisa ambao hawatafikia vigezo hivyo watalazimika kubaki katika vitengo vingine vya ulinzi wa taifa lakini pia wanakabiliwa na tishio la kufutwa kazi kwasababu kuna mpango wa kuunganisha idara ya polisi na vitengo vingine vya ulinzi kufikia mwisho wa mwezi Juni.
Taarifa hiyo ilifichuka baada ya kanda ya rekodi yenye sauti ya kamanda wa polisi Raúl Ávila Ibarra, iliyovujishwa kupatikana na gazeti la El Universal.
Katika kanda hiyo afisa huyo wa ngazi ya juu anasikika akijaribu kuwashawishi maafisa wadogo kujiunga na na kitengo kipya cha huduma ya uhamiaji huku akiwaelezea kuwa kitengo hicho kipya kinalipa vizuri kuliko chao polisi ".
"Wengine wetu tulio na uzani mkubwa tuna hadi miezi sita kubuni mbinu ya kufukia masharti tuliyopewa," Bw. Ávila Ibarra alisikika akisema.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment