Search This Blog
Monday, June 3, 2019
Dk. Kalemani atoa agizo TANESCO
Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani ameliagiza Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kuhakikisha mitaa yote kwenye majiji, inapatiwa umeme ifi kapo Juni 30, mwaka huu.
Kauli hiyo aliitoa mara baada ya kufanya ziara kutembelea maeneo ya Mkonze na Ntyuka katika Jiji la Dodoma, ambayo yana nyumba ambazo hazijaunganishiwa umeme.
Dk Kalemani alisema mitaa yote katika jiji hilo, inatakiwa kuwa na umeme ifikapo tarehe hiyo, kwani maeneo hayo yana kero kubwa ya kupata umeme ijapokuwa yapo jijini.
Alisema maeneo hayo lazima yapatiwe umeme haraka ili yafanane na hadhi ya jiji. Dk Kaleman alitaka wataalamu kutoka Tanesco kutokataa malipo ya wananchi, wanaotaka kuunganishiwa umeme, bali wanapaswa kuyapokea malipo hayo na kuharakisha kuwasambazia umeme wateja hao.
Kabla ya kufanya ziara hiyo, Dk Kalemani akizungumza katika kikao na watendaji wa Tanesco na kuwataka kushughulikia kwa haraka suala la kuwaunganishia umeme wananchi waliolipia.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment