INADAIWA beki kisiki wa Yanga, Andrew Vincent ‘Dante’ anawaniwa na mabingwa wa Kombe la Shirikisho (FA), Azam FC ambayo msimu ujao itashiriki Kombe la Shirikisho Afrika.
Dante amekuwa mmoja kati ya mabeki wa kati wa Yanga waliofanya vizuri msimu wa 2018/19 kwa kushirikiana na beki mkongwe Kelvin Yondani.
Habari za ndani zinadai kuwa nyota huyo anawindwa na Azam pamoja na timu nyingine kutoka nje ya Tanzania.
Hata hivyo, beki huyo inadaiwa bado Yanga inahitaji kubaki naye ili kuongeza nguvu kwenye safu ya ulinzi kwa msimu ujao.
Kwa upande wa Azam kupitia kocha Abdul Mingange, alisema: “Suala la usajili kwa sasa ni mapema kulizungumzia, ripoti yangu nitakabidhi kwa uongozi na kila kitu kitajulikana.”
Search This Blog
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment