Search This Blog

Tuesday, May 28, 2019

Waziri Kanyasu awapa agizo hili TAWA


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu ameiagiza Mamlaka ya  Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) iunde timu ya kuchunguza uhalali wa malipo ya kifuta jasho na kifuta machozi kilichotolewa kwa wananchi  walioathiriwa  na wanyamapori wakali na waharibifu wa mazao katika maeneo mbalimbali nchini.

Mhe. Kanyasu ametoa agizo hilo mara baada ya kupokea malalamiko na madai kutoka kwa baadhi ya wananchi wa vijiji 4 vinavyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, wilayani Bunda mkoani Mara ambao  mazao yao yaliliwa na kuharibiwa na wanyamapori wakali wamekuwa hawalipwi  huku wasiostahili ndo wamekuwa wanalipwa .

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vijiji vya Sarakwa, Mariwanda ,Unyali na Kihomboi vinavyopakana na  Hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Bunda mkoani Mara, Mhe.  Kanyasu amesema  kuwa mara  baada ya uchunguzi kukamilika wale watakaobainika kupokea fidia hiyo wale wasiostahili watachukuliwa  hatua kali za kisheria ikiwemo kuzirudisha fedha hizo.

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...