Search This Blog
Monday, May 27, 2019
Utabiri mpya wa babu wa Loliondo
Takribani miaka 9 tangu kupungua kwa idadi ya watu waliokuwa wakifika katika kijiji cha Samunge, tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro Mkoani Arusha kupata kikombe cha Babu, mchungaji aliyekuwa akitoa huduma hiyo Ambilikile Mwaisapile ameibuka tena na kutoa utabiri mpya.
Mchungaji Mwasapile amesema kwamba Tanzania inaenda kuwa kioo na taifa la mfano ambapo mataifa mengi kote duniani yatafika hapa nchini kujifunza mambo mbalimbali.
Akizungumzia kupungua kwa idadi ya watu wanaofikia kupata kikombe Mchungaji Ambilikile amesema kunachangiwa na uvumi uliopo kuwa Babu wa loliondo alishafariki huku baadhi ya watu wakionekana bado wakiendelea kufurahia huduma ya kikombe.
Ikumbukwe kwamba kati ya mwaka 2010 na mwaka 2011 huduma ya kikombe cha babu ilivuta maelfu ya watu kutoka kila kona ya nchi kwa kile kilicho aminika kutibu maradhi sugu ya mwili.
http://bit.ly/2HWQXfp
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment