Search This Blog

Monday, May 27, 2019

Utabiri mpya wa babu wa Loliondo


Takribani miaka 9 tangu  kupungua kwa idadi ya watu waliokuwa wakifika katika kijiji cha Samunge, tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro Mkoani Arusha kupata kikombe cha Babu, mchungaji aliyekuwa akitoa huduma hiyo Ambilikile Mwaisapile ameibuka tena na kutoa utabiri mpya.

Mchungaji Mwasapile amesema kwamba Tanzania inaenda kuwa kioo na taifa la mfano ambapo mataifa mengi kote duniani yatafika hapa nchini kujifunza mambo mbalimbali.

Akizungumzia kupungua kwa idadi ya watu wanaofikia kupata kikombe Mchungaji Ambilikile amesema kunachangiwa na uvumi uliopo kuwa Babu wa loliondo alishafariki huku baadhi ya watu wakionekana bado wakiendelea kufurahia huduma ya kikombe.

Ikumbukwe kwamba kati ya mwaka 2010 na mwaka 2011 huduma ya kikombe cha babu ilivuta maelfu ya watu kutoka kila kona ya nchi kwa kile kilicho aminika kutibu maradhi sugu ya mwili.

http://bit.ly/2HWQXfp

No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...