Search This Blog
Thursday, May 23, 2019
Uchaguzi wa bunge la Ulaya waanza Uholanzi na Uingereza
Jumla ya wapiga kura milioni 400 wanatarajiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo katika nchi 28 wanachama wa umoja huo. Jumla ya wabunge au wawakilishi 751 kuchaguliwa.
Uchaguzi wa bunge la Ulaya umeanza leo. Uholanzi na Uingereza ndizo nchi ambazo wapigakura wao wanashiriki leo kuwachagua wawakilishi wao katika bunge hilo. Jumla ya nchi 28 wanachama zinatarajiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo utakaodumu kwa siku nne.
Nchi mbili pekee ndizo zinafanya uchaguzi wa bunge la Ulaya kwa siku ya leo zikiwa ni Uholanzi na Uingereza.
Nchini Uholanzi, vituo vya upigaji kura vilifunguliwa mapema na nusu saa baadaye zoezi hilo pia likaanza Uingereza, nchi ambayo inakabiliwa na msukosuko wa kupata muafaka wa kujiondoa katika Umoja wa Ulaya.
Jumla ya wapiga kura milioni 400 wanatarajiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo katika nchi 28 wanachama wa umoja huo. Jumla ya wabunge au wawakilishi 751 wanatarajiwa kuchaguliwa kwenye uchaguzi huo unaotajwa kuwa miongoni mwa chaguzi za kidemokrasia zaidi ulimwenguni.
Nchini Uingereza, kura ya maoni inaonyesha kuwa chama kipya cha Brexit kitapata ushindi wa kati ya asilimia 30-40 za kura dhidi ya vyama viwili vikuu, kinachotawala cha kihafidhina ‘Conservatives' na kile cha upinzani ‘Labour.'
Wafuasi wa zamani wa chama cha waziri Mkuu Theresa May, wanatarajiwa kukiunga mkono chama cha Brexit, kutokana na mkwamo uliopo wa Uingereza kushindwa kujiondoa katika Umoja wa Ulaya na kusababisha wao kushiriki uchaguzi huo.
http://bit.ly/2Wq3cKq
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment