Search This Blog
Thursday, May 23, 2019
Spika Ndugai awataka Wabunge wampuuze Masele
Spika wa Bunge, Job Ndugai ameliomba Bunge limsamehe na kumpuuza Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Afrika (PAP) na Mbunge wa Shinyanga Mjini, Stephen Masele ambaye anatuhumiwa kwa kutokuwa na nidhamu kwa kuichonganisha Serikali na Bunge.
Spika Ndugai aliitaka Kamati ya Haki, Madaraka na Maadili Jumatatu, Mei 20, kumhoji Mbunge huyo na leo, kamati hiyo imetoa taarifa ya kumsamehe mara baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu.
“Bunge katika uendeshwaji wake ni lazima tuangalie vikao vingine vya bunge vilivyopita, mambo yaliyotokea na kwa muda mrefu hakukuwahi kutokea mambo kama haya.
“Mheshimiwa Samweli Sitta, katika mazingira kama haya aliwahi kuliomba bunge kumpuuza mbunge fulani, kwa maana hiyo nami nawaomba tumpuuze Masele na tumsamehe, tuendelee na mambo ya maana, hatuna ubaya na mtu yeyote,” amesema Ndugai.
Aidha Spika huyo amewataka wabunge kuacha kupeleka maneno ya umbea kwa Rais Dk John Magufuli kwa kuwa maneno hayo yanamyumbisha na kumchanganya Rais katika utendaji wa kazi zake.
“Muoneeni huruna mheshimiwa Rais, anafanya kazi kubwa sana acheni kupeleka umbea, uwongo na fitina kwaRrais tunamyumbisha, tunamchanganya na kumzeesha acheni kuwagombanisha Waziri MKuu na Spika migongano ya nini, nilipeleka hiki kwa viongozi wangu, nilipeleka hivi, uchonganishi mtupu hamna ukweli wowote.
“Tuache hiyo tabia, unajambo njoo kwa spika wewe ni mbunge unaweza kuchukua wabunge wenzio wenye heshima zao mje kwa Spika, sema jamani mimi Spika hanitendei mema tutaelewana tuu acheni ushabiki wakupiga piga makofi,” amesema Spika.
http://bit.ly/2M2pG0c
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment