Search This Blog
Friday, May 24, 2019
TAKUKURU yawashikiria watu watatu, Diwani wa Ukonga ndani
Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa nchini (TAKUKURU), inawashikilia watu watatu akiwamo Diwani wa Kata ya Ukonga (Chadema), Jumaa Mwipopo na Ofisa Mtendaji was kata hiyo, Rozalia Silumbe kwa tuhuma za kuomba Rushwa ya Sh.400,000 kwa mwananchi aliyekuwa anatuhumiwa kufanya uharibifu wa mazingira.
Akizungumza na Waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Ilala, Christopher Myava amesema, watuhumiwa hao walikamatwa Mei 22, mwaka huu, saa 9 alasiri, Katika ofisi za Kata ya Ukonga.
Amesema watuhumiwa hao walishawishi na kuomba Rushwa ya Sh.400,000 na kupokea Sh.300,000 kutoka kwa mwananchi huyo.
“Watuhumiwa watafikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kujibu tuhuma chini ya kifungu Cha 15 (1) (a)Cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na.11/2007,”amesema Myava.
Aidha Takukuru imewatahadhalisha wananchi kuacha kurubuniwa na matapeli na badala yake watoe taarifa mapema.
http://bit.ly/2WYpQXv
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment