Search This Blog
Saturday, May 25, 2019
RC Mahenge awatahadharisha watendaji juu ya fedha za vitambulisho vya JPM
Na.Enock Magali,Dodoma
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt,Binilith Mahenge amewatahadharisha watendaji wa kata pamoja na wale wote waliopewa jukumu la kuuza vitambulisho vilivyotolewa na Rais Dkt.John Pombe Magufuli kwa ajili ya wajasiriamali kutothubutu kuzitumia fedha watakazo kuwa wamekusanya kwa matumizi yao binafsi kwani zitawagharimu.
Dkt.Mahenge ameyasema hayo Wilayani Kondoa katika muendelezo wa ziara yake ya kukagua,kugawa,kutoa elimu na kuhamasisha wajasiriamali walio chini ya mtaji wa Shilingi Milioni nne kuwa na vitambulisho hivyo.
Akizungumza na watumishi mbalimbali wa Wilaya hiyo,amewataka kuwa waangalifu na fedha wanazozipata kutokana na mauzo ya vitambulisho hivyo.
"Kuweni makini sana na vitambulisho hivyo,fedha mnayoipata iwasilisheni sehemu husika kwa uaminifu,hali ni mbaya mno msiziguse kabisa"Alisema
Aidha pia Dkt.Mahenge amegawa vitambulisho kwa wakuu wa Idara pamoja na watendaji wa kata zote za wilaya hiyo,huku akiwasisitiza kuongeza juhudi katia kuvisambaza kwa wafanyabiashara na kutomruhusu mtu yeyote kufanya biashara pasi kuwa na kitambulisho.
"Mtu ambaye hana kitambulisho haruhusiwi kufanya biashara,kila anaye fanya biashara ni lazima awe kwenye makundi mawili,kundi la kwanza ni lazima awe na leseni ya biashara na pili ni lazima awe na kitambulihso cha wajasiriamali na ni lazima akivae muda wote wa kazi,simamieni hili.Alisisitiza.
Na katika wakati huo huo amewataka wananchi wa Mkoa wa Dodoma kutii agizo na maelekezo ya Serikali juu ya katazo la matumizi ya mifuko ya Plastiki linaloanza kutekelezwa rasmi June Mosi mwaka huu.
http://bit.ly/2wlhpty
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment