Search This Blog
Saturday, May 25, 2019
Ushoga kuendelea kuwa kosa la jinai Kenya
Mahakama kuu nchini Kenya imeamua sheria inayopinga mapenzi ya jinsia moja itaendelea kutumika nchini kinyume na ilivyotarajiwa na wanaharakati waliotaka ifutiliwe mbali.
Katika uamuzi huo, majaji wameamua kwamba sheria inayopingwa, maarufu kanuni 162 hailengi makundi yoyote maalum ya watu na badala yake inaeleza kwamba ni makosa kwa yoyote kushiriki katika uhusiano wa aina hiyo.
Mahakama imeeleza kwamba inatambua umuhimu wa haki za binaadamu hatahivyo, imeeleza kwamba sheria imeweka mpaka au ukomo kwa baadhi ya haki hizo.
Uamuzi huo uliosubiriwa kwa muda mrefu umetazamwa kwa umuhimu mkubwa kwa jamii ya wapenzi wa jinsia moja (LGBT) nchini.
Wanaharakati wamekuwa wakilalamika kwamba sheria hiyo, inakiuka katiba ya mwaka 2010 nchini inayohakikisha usawa, heshima na faragha kwa raia wote.
Kwa mujibu wa sheria nchini Kenya, mtu anayepatikana kujihusisha katika mahusiano ya jinsia moja anaweza kuhukumiwa miaka 14 gerezani.
Katika utangulizi wake Hakimu Roselyn Aburili ameeleza kwamba ni muhimu na ni jukumu la mahakama kuheshimu maadili ya kitaifa na kwamba vifungu vya sheria ni muhimu viambatane na katiba nchini.
http://bit.ly/2QloO5m
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment