Search This Blog
Monday, May 27, 2019
Kinyang'anyiro cha kuwania Uwaziri Mkuu wa Uingereza chapamba moto
Kinyang'anyiro cha kuwania wadhifa wa waziri mkuu wa Uingereza kimepamba moto, baada ya hivi leo Waziri wa Mazingira Michael Gove kujiunga na orodha ndefu ya wanasiasa wanaotaka kumrithi Theresa May aliyejiuzulu Ijumaa iliyopita.
Wanasiasa waliokwishatangaza kuwania wadhifa huo wana mitazamo inayotofautiana juu ya namna Uingereza itakavyojitoa Umoja wa Ulaya.Kujiuzulu kwa Bibi May kumeongeza uwezekano wa Uingereza kuondoka kutoka Umoja huo bila ya mkataba ifikapo Oktoba 31, ambayo ni tarehe ya mwisho iliyowekwa na viongozi wa Umoja wa Ulaya.
Miongoni mwa wagombea wanane wanaotaka kumrithi May wamesema watajaribu kutafuta mabadiliko kwenye mkataba uliofikiwa na Umoja wa Ulaya mwaka uliopita lakini wanajiweka tayari kwa uwezekano wa kuiondoa Uingereza bila mkataba wowote iwapo juhudi zao zitakataliwa.
Umoja wa Ulaya umesema hautojadiliana upya vipengele vya mkataba uliofikiwa na waziri mkuu anayeondoka madarakani.
http://bit.ly/2VS7hD5
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment