Search This Blog
Sunday, May 26, 2019
Apigwa faini kwa kujikuna huku anaendesha gari
Mwanaume mmoja kutoka mashariki mwa China amepigwa faini mara baada ya kamera ya trafiki kumpiga picha akiwa anajikuna usoni.
Kwa mujibu wa chapisho la Jilu Evening, limeandika kuwa Liu alikuwa anaendesha gari siku ya jumatatu katika jimbo la Shandong na huku akiwa anajikuna wakati anapita katika kamera ya trafiki.
Ghafla alipokea ujumbe unaomwambia kuwa amevunja sheria barabarani kwa kuendesha gari huku anaongea na simu.
Picha ya kosa ambalo alikuwa amelifanya liliambatanishwa katika ujumbe huo wa kuvunja sheria.
Aliambiwa kuwa ataondolewa pointi mbili katika leseni yake na vilevile alitakiwa kulipa dola saba kama faini.
"Huwa nawaona watu mitandaoni wakiwa wamekatwa kwa kosa la kuendesha huku wamewashika watu wengine labda miguu lakini mimi nimekamatwa kwa kujishika mwenyewe ndio nimeonekana kuwa nimevunja sheria, inashangaza'!"
Mshitakiwa huyo amesema kuwa anajaribu kuongea na mamlaka ili kupata suluhisho ya tatizo lake .
http://bit.ly/2QkLkey
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Punguza kilo tano kwa siku saba
NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...
-
Kiwanja kinauzwa kipo Dodoma Mahungu njia ya kwenda Singida kabala hujafika NALA. Kiwanja ni cha Makazi kinaukubwa wa Sqm 450 ( 15 X...
-
Akionekana kwa mara ya kwanza kwa umma tangu aondoke madarakani, aliyekuwa Rais wa Marekani Donald Trump ameweka wazi uwezekano wa kuwania...

No comments:
Post a Comment