Search This Blog

Friday, October 22, 2021

Nigeria yasitisha huduma ya reli baada ya shambulio



Shirika la reli la Nigeria limesitisha kwa muda huduma za reli kutoka Abuja, kuelekea kaskazini magharibi mwa Kaduna baada ya watu wenye silaha kuwavamia abiria wa treni siku ya Jumatano.

Watu walioshuhudia walisema washambuliaji hao walimlenga dereva wa treni ingawa hakuna majeruhi alireripotiwa mpaka sasa.

Abiria mmoja aliiambia BBC kuwa walisikia mlio mkubwa kabla ya treni haijasimama kwa saa kadhaa.

Mbunge wa zamani nchini humo, Senata Shehu Sani, aliandika kwenda tweeter kuwa treni ya pili na hivyo kulazimika kurudi Abuja siku ya Alhamisi baada ya mlipuko ulipotokea katika reli hiyo.

Kampuni ya reli ya Nigeria ilisema huduma hizo zitarudi baada baada ya Ijumaa baada ya ukarabati..

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...