Search This Blog

Friday, October 22, 2021

Li Hyundai: Mpiga piano maarufu wa China azuiliwa kwa ‘kutumia huduma za kahaba’


Mpiga piano wa maarufu nchini China Li Yundi amezuiliwa kwa kutumia huduma kahaba, vyombo vya habari vya serikali vinasema.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 39 na msichana mwenye umri wa miaka 29, wamekiri kwa shughuli hiyo haramu, polisi wa Beijing walisema katika chapisho mtandaoni . Walikamatwa baada ya mamlaka kupokea dokezo kutoka kwa umma.

Ingawaje polisi hawakuchapisha jina lake kamili katika ilani hiyo, vyombo vya habari vya serikali baadaye vilithibitisha kuwa ni Li.

Habari hiyo imewashtua mashabiki wake wengi na nchini China anafahamika kama "Piano Prince".

Akiwa na miaka 18 tu, Li alikua mpiga piano mchanga zaidi - na mtu wa kwanza kutoka china - kushinda tuzo ya kwanza kwenye Mashindano ya kifahari ya Kimataifa ya Chopin Piano mnamo 2000.

Ameendelea kutumbuiza kote ulimwenguni na ni jina linalotambulika sana katika maeneo yanayozungumza Kichina



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...