Search This Blog

Tuesday, October 19, 2021

Mtu aanguka kutoka katika puto na kufariki Israel


Mtu mmoja amefariki kaskazini mwa taifa la Israel baada ya kuponyoka kutoka kwa puto au kibofu na kuanguka juu ya gari lililokuwa likiendeshwa.


Vyombo vya habari vya Israel viliripoti kwamba , mtu huyo ambaye yuko katika mwenye umri wa miaka 20alikuwa mfanyakazi wa ardhini ambaye alikuwa akibembea katika kapu la puto hilobaada ya kupaa.


Abiria wa puto hilo walijaribu kumvuta ndani , lakini aliponyoka na kuanguka yapata mita 100 hadi katika gari lililokuwa likiendeshwakatika barabara kuu karibu na mji wa Afula.


Maafisa wa afya walisema kwamba mtu huyo alifariki papo hapo baada ya kuanguka. Watu waliokuwa ndani ya gari hilo hawakuhitaji matibabuhuku abiria waliokuwa katika puto hilo wakitua salama salmin.


Tukio hilo litachunguzwa na maafisa wa polisina maafisa wa mamlaka ya angani nchini humo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...