Ripoti mpya inasema kuwa Afrika inahitaji hadi dola bilioni 50 kwa mwaka ili kukabiliana natisho linaloongezeka la mabadiliko ya hali ya hewa climate change.
Jumuiya ya Afrika na Shirika la Hali ya Hewa Duniani zinaonya kuwa karibu watu milioni 120 maskini wanakabiliwa na tishio la mafuriko, ukame, makazi yao, na joto kali ifikapo mwishoni mwa muongo huu ikiwa hatua madhubuti hazitachukuliwa.
Pia inaonya kuwa barafu zilizosalia za barani Afrika ziko zinaelekea kutoweka ifikapo miaka ya 2040.
Afrika imeathiriwa na mabadiliko ya tabia nchi ijapokuwa inawajibikia asilimia nne tu uzalishaji wa chafu duniani.
No comments:
Post a Comment