Search This Blog

Monday, October 18, 2021

Msaidizi wa karibu wa Rais wa Venezuela ashtakiwa Marekani



Mmoja wa wasaidizi wa karibu wa Rais wa Venezuela Nicolás Maduro amesafirishwa kutoka Cape Verde kwenda Marekani, ambapo ameshtakiwa kwa utakatishaji fedha.

Hazina ya Marekani inasema Alex Saab alifkuwa kiungo muhimu wa serikali ya Bwana Maduro.

Serikali ya Venezuela imesitisha mazungumzo yake na mrengo na upinzani ambao unaungwa mkono na Marekani.

Mazungumzo hayo yalikuwa ya kutatua mgogoro wa kisiasa ambao umesababisha vurugu na kuporomoka kwa uchumi.

Majadiliano hayo yalipaswa kuanza tena wikendi hii huko Mexico.

Marekani inamshutumu Bwana Saab - mfanyabiashara mzaliwa wa Colombia na mjumbe wa Venezuela - kwa kutumia akaunti zake katika benki za Marekani ili kupata mapato ya ufisadi.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...