Search This Blog

Monday, October 18, 2021

Abiy: Ethiopia lazima isimamishe msaada wa chakula ili kuepuka shinikizo

Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed anasema nchi hiyo inahitaji kukoma kupokea msaada wa chakula ili kuepuka shinikizo za kigeni dhidi ya serikali, Kituo cha televisheni cha kinachomilikiwa na serikali ETV) kimeripoti.

"Tukihakikisha vitu hivi vinavyoitwa ngano [msaada wa chakula] haviingii Ethiopia, asilimia 70 ya matatizo ya Ethiopia yatasuluhishwa.

"Tatizo la Ethiopia ni msaasa wa ngano. Kutokana na msaaada wa ngano kunakuja magonjwa. Kutokana na masaada wa ngano kunakuja mambo mengi, athari nyingi. Tukisimamisha, baadhi ya matatizo yatasuluhishwa ," Bwana Abiy alisema.

Waziri Mkuu alisema hayo alipozuru mashamba ya ngano katika eneo la Oromia.

Ethiopia, ambayo ni miongoni mwa nchi ambazo zinapokea misaada ya kigeni, inakabiliwa na shinikizo kutoka kwa nchi kadhaa za magharibi kutokana mzozo wa Tigray kaskazini mwa nchi, ambako ambapo mamilioni wako katika hatari ya njaa.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...