Search This Blog

Friday, October 8, 2021

Mchezaji filamu maarufu wa Nigeria Chiwetalu Agu akamatwa


Jeshi la Nigeria limethibitisha kumkamata mchezaji wa filamu wa N Nollywood Chiwetalu Agu.

Kulingana na taarifa kutoka makao makuu ya jeshi wamemkamata wakati walipokuwa wakifanya msako wa wafuasi wa genge linalounga mkono jamii ya wazawa ya Biafra wanaotaka kujitenga nchini humo (IPOB).

Taarifa hiyo imeeleza pia kwamba mchezji filamu huyo alichukuliwa alipokuwa amefaa nguo zinazotambulisha kikundi hicho kwa ajili ya kumuhoji na ingawa alionyesha pingamizi, jeshiu limefanya juhudi za kumuweka mahabusu , na linasema halikumyamyasa wala kumtesa.

Taarifa hikyo imeongeza kuwaingawa jeshi linatambua haki za raia wote za kutembea kwa uhuruna kujieleza kama haki yao ya kikatiba, halitakubali ukiukaji wa wa sheria wa mtu binafsi au kikundi kwa kuchochea umma kufanya ghasia au kuvunja sheria na utulivu.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...