
Waziri wa mambo ya nje wa Mali amemuita balozi wa Ufaransa Jumanne kupinga kauli zilizotolewa na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kuhusu serikali inayoongozwa na jeshi.
Wizara ya mambo ya nje ilisema kuwa ilikuwa imemuita balozi wa Ufaransa kumfahamisha juu ya ' 'ghadhabu na kutokubali'', kwa kauli zilizonukuliwa na mashirika ya habari.
Jumanne Rais Macron aliwashutumu maafisa wa kijeshi wa Mali kwa kuacha kutekeleza majukumu yao.
Aliviambia vyombo vya habari kuwa sio jukumu la jeshi la Ufaransa kujazi kile alichokielezea kama "mambo yasiyo ya kazi ‘’ ya taifa la Mali.
"Waziri huyoaliwataka maafisa wa Ufaransa kuwa na subira, kuepuka kutoa kuhukumu," imesema Wizara ya mambo ya nje ya Mali.
Mwezi uliopita, waziri mkuu wa mpito wa Mali, Choguel Maïga, iliishutumu Ufaransa kwa "kulitelekeza" taifa katika kile alichosema "katikati ya safari ya angani" baada ya nchi hiyo ya Ulaya kuamua kupunguza nusu ya vikosi vyake nchini Mali.
Uhusiano baina ya nchi mbili umeharibika tangu yalipofanyika mapinduzi ya kijeshi nchini Mali mwaka jana.
No comments:
Post a Comment