Search This Blog

Thursday, October 21, 2021

Kiongozi wa vuguvugu la kujitenga Nigeria kufikishwa mahakamani leo


Kesi dhidi ya kiongozi wa vuguvugu la kujitenga nchini Nigeria Nnamdi Kanu inarejelewa leo mjini Abuja

Bwana Kanu ni kiongozi wa kundi la Indigenous People of Biafra (Ipob), kundi linalotaka kujitenga kwa jimbo la kusini -mashariki mwa Nigeria, ambalo serikali imeharamisha. Anakabiliwa na mashataka ya "ugaidi na uhaini.

Akipatikana na hatia huenda akafungwa maisha. Nnamdi Kanu amekua akizuiliwa na polisi wa kisiri kulingana na mawakili wake.

Wiki iliyopita serikali ya Nigeria imefanyia marekebisho mashataka dhidi yake na kuongeza kuwa anaendesha kampuni haramu na kuchapisha taarifa za kuchafua sifa.

Hali ya taharuki ilipanda mwezi Julai wakati amamlaka ilipokosa kumfikisha mahakamani kumfungulia mashataka.

Mawakili wake wanataka serikali kuhakikisha anafikishwa mahakamani leo.

Wanachama wa kundil lake linalotaka kujitenga kwa eneo la Biafra, have been agitating for a breakaway state for the southeast region of the country.

Kanu alikamatwa mara ya kwanza Oktoba 2015, lakini akatoroka Nigeria 2017 baada ya jeshi kuvamia nyumbani kwake.

Alikamatwa mwezi Juni mwaka huu. Mawakili wake walishutumu serikali kwa kukiuka sheria za kimataifa na kukiuka haki zake.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...