Search This Blog

Saturday, October 2, 2021

Hii hapa ratiba ya ligi kuu leo


LIGI Kuu Tanzania Bara inaendelea leo ikiwa ni mzunguko wa pili kwa timu kuendelea kupambania pointi tatu ndani ya uwanja.

Oktoba 2 viwanja vitatu vitakuwa na kazi ya kuonyesha shughuli ya timu hizo katika kusaka ushindi.

Coastal Union ya Tanga iliyotoka kulazimisha sare ya kufungana bao 1-1 dhidi ya Azam FC leo inawakaribisha KMC, Uwanja wa Mkwakwani.


KMC imetoka kupokea kichapo mbele ya Polisi Tanzania kwenye mchezo uliochezwa Uwanja wa Karatu, Arusha.

Polisi Tanzania itakutana na Azam FC kwenye mchezo utakaochezwa Uwanja wa Ushirika, Moshi.

Yanga ambao walitoka kushinda bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar wanakibarua cha kusaka ushindi mbele ya Geita Gold, Uwanja wa Mkapa na itakuwa ni saa 1:00 usiku.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...