Search This Blog

Wednesday, September 8, 2021

Zimbabwe yawataka wafanyakazi wa serikali kupokea chanjo au kujiuzulu

 


Serikali nchini Zimbabwe imewataka wafanyakazi wake kupata chanjo dhidi ya Covid-19 au wajiuzulu.

Inasema hatua hiyo inalenga kupunguza hatari ya kueneza virusi.

Katika mahojiano na kituo cha redio cha eneo hilo, Waziri wa Sheria Ziyambi Ziyambi anasema kuwa wafanyikazi ambao wanafikiria wana haki ya kuchagua ikiwa wanaweza kupewa chanjo au la wamekosea

Serikali mapema ilianzisha kanuni mpya kwa makanisa na mikahawa ili kuruhusu tu watu walio na kadi ya chanjo ndani ya majengo yao.

Lengo ni kukabiliana na changamoto ya watu kusita kuchanjwa .

Nchi hiyo ya kusini mwa Afrika imeweza kutoa chanjo kamili kwa watu milioni 1.7 pekee



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...