Search This Blog

Monday, September 20, 2021

Yanga yarejea salama Dar


KIKOSI cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi leo Septemba 20 kimewasili salama katika ardhi ya Tanzania kikitokea nchini Nigeria.

Mabingwa hao mara 27 wa Ligi Kuu Tanzania Bara walikuwa wakipambana kwa ajili ya kupeperusha bendera kimataifa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

Deni lao kubwa ilikuwa ni kwenye kupindua meza kibabe mbele ya Rivers United kwa sababu katika mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Mkapa ubao ulisoma Yanga 0-1 Rivers United hivyo walitakiwa kushinda mabao zaidi ya mawili.

Yanga ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Rivers United pia jana na mchezo ulipokamilika walianza safari kurudi Tanzania. 


Ni Shirika la Ndege la Tanzania walitumia ndege bora na wameweza kurudi salama Tanzania leo Septemba 20.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...