Search This Blog

Monday, September 20, 2021

Hukumu dhidi ya Rusesabagina kutolewa leo Rwanda


Mahakama mjini Kigali leo inataraji kutoa hukumu yake dhidi ya Paul Rusesabagina, mkosoaji mkuu wa serikali ya Rwanda.

Yeye na washirika wenzake 20, watuhumiwa kwa ugaidi ambao unaunahusiana wa mashambulio yaliyofanywa na kundi la waasi la MRCD- FLN dhidi ya Rwanda miaka ya 2018 na 2019.

Waendesha mashtaka waliomba hukumu ya kifungo cha maisha jela dhidi ya Rusesabagina aliyejitoa katika kesi hiyo mara tu ilipoanza kusikilizwa kwa madai kuwa hawezi kupata haki katika mahakama za Rwanda.

Juhudi za Bwana Paul Rusesabagina ambaye ni mwanahotelia wa zamani zilisaidia kuwaokoa zaidi ya watu 1200 wakati wa mauaji ya kimbari nchini humo ziliangaziwa katika filamu ya Marekani, Baadaye alikuwa mkosoaji wa serikali ya Rais Paul Kagame.

Aliishia kushtakiwa na kufungwa nchini Rwanda baada ya kudaiwa kutekwa mjini Dubai. Rwanda imekanusha kumteka.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...