Search This Blog

Friday, September 3, 2021

Uganda inamshikilia msomi wa Rwanda kwa tuhuma za ujasusi


Vikosi vya usalama nchini Uganda vinamshikilia Makamu mkuu wa chuo Kikuu cha kibinafsi -Victoria University kwa madai ya ujasusi na kuishi nchini humo kinyume cha sheria, amesema msemaji wa jeshi Brigadia Jenerali Flavia Byekwaso.

Dkt. Lawrence Muganga, ambaye ni mzaliwa wa Rwanda alichukuliwa na maafisa ambao hawakuwa wamevaa sare kutoka katika ofisi yake mjini Kampala Alhamisi mchana.

Haijulikani iwapo kukamatwa kwake kuna uhusiano na Rwanda, ambayo ni nchi jirani na Uganda.

Mahusiano baina ya nchi hizo mbili wakati mwingine huwa ya wasi wasi- huku pande mbili zikilaumiana kila upande kuingilia maswala ya ndani ya nchi ya mwenzake.

Jenerali Byekwaso aliiambia BBC kwamba uchunguzi ulikuwa umeanza.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...