Search This Blog

Friday, September 3, 2021

Muungano wa Ulaya kurudisha mamilioni ya chanjo za corona Afrika


Muungano wa Ulaya utarudisha mamilioni ya dozi ya chanjo za Johnson & Johnson zilizotengenezwa Afrika Kusini katika bara la Afrika.

Mjumbe maalum wa Muungano wa Afrika Strive Masiyiwa amewambia waandishi wa habari kwamba chanjo zote zinazotengenezwa “zitabakia Afrika na kusambazwa Afrika”.

“Swala limerekebishwa na limerekebishwa kwa njia chanya ,” amesema.

Hii inafuatia ukosoaji kwamba chanjo zinasafirishwa kutoka bara la Afirka ambalo lina viwango vya chini vya uchanjaji duniani.

Chini ya asilimia 3 ya idadi ya watu wa Afrika ndio waliochanjwa chanjo dhidi ya Covid-19.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...