Rais wa Burundi, Evariste Ndayishimiye, ameshutumiwa kwa kumshambulia kwa maneno mwandishi wa habari aliyeangazia hali ya ugonjwa wa corona nchini humo.
Rais alikuwa amesema Esdras Ndikumana, ambaye ni mwanahabari wa kituo cha Ufaransa RFI, alikuwa akichafua taswira ya Burundi kutokana na habari yake.
Hata hivyo, Waandishi Wasio na Mipaka (RSF) walisema kuwa "matamshi hayo yana uzito mkubwa na hatari" ni "ukumbusho wa kusikitisha wa uhuru wa vyombo vya habari jinsi ulivyo dhaifu nchini Burundi."
Shirika la habari la RFI lilielezea "tuhuma za rais kama "zisizo na msingi na za kipuuzi."
Mkuu wa RSF Afrika Arnaud Froger alimsihi rais " kutotengeneza uadui pasipo na haja" na kuongeza kwamba anachostahili kufanya ni "kupambana na janga hilo badala ya kukabiliana na waandishi wa habari".
Siku za nyuma, kumekuwa na wasiwasi juu ya uhuru wa vyombo vya habari nchini Burundi.

No comments:
Post a Comment