Search This Blog

Monday, September 20, 2021

Papa afungua kongamano la mgogoro wa unyannyasaji wa kingono kwa watoto


Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis, jana Jumapili amefungua kongamano lenye kuhusu makabiliano ya unyanyasaji wa kingono dhidi ya watoto, unakodaiwa kufanya na makakisi katika eneo la Ulaya ya Kati na Mashariki, nchini Poland. 
 
Katika hafla hiyo ya ufunguzi Papa amewataka washiriki kusugua kichwa katika kufanikisha upatikanaji wa njia thabiti ya mageuzi. Kongamano hilo linalofanyika mjini Warsaw linawakatunaisha washiriki kutoka mataifa 20 tofauti. 
 
Kanisa Katoliki lenye ushawishi mkubwa wa kisiasa nchini Poland, limekuwa katika mtikisiko baada ya kukumbwa na mfululizo wa kashfa za ngono. Tangu mwaka uliopita makao makuu ya kanisa hilo Vatican yamewawekea vikwazo maaskofu 8 wa kwa kufikwa na kashfa hizo.
 
 Aidha kanisa hilo nchini Polanad lilitangaza kuanzia Julai 2018 hadi kufikia mwishoni mwa 2020, limepokea tuhuma 368 za unyanyasaji wa kingono ambao umedaiwa kufanywa na makasisi.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...