Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amemkosoa mgombea wa ukansela wa chama cha SPD Olaf Scholz kwa utayari wake wa kushirikiana na chama cha Die Linke.
Merkel amemshambulia Scholz, ambaye pia ni waziri wa fedha, baada ya mgombea huyo kusema hapingi uwezekano wa kuunda muungano na chama cha siasa kali za mrengo wa kushoto Die Linke, baada ya uchaguzi.
Chama cha kihafidhina cha Christian Democratic Union CDU cha Angela Merkel, kimepinga wazo la muungano na chama cha Die Linke kutokana na kile inachokitaja kuwa chama hicho cha siasa kali kina sera ya kigeni isiyokubalika.

No comments:
Post a Comment