Maofisa watano wa wizara ya mambo ya ndani nchini Afrika Kusini wamesimamishwa kazi kwa kuwa walishiriki katika kumsaidia mchungaji wa Malawi kwenye nakala za makazi.
Mchungaji Shepherd Bushiri alipata kibali cha makazi cha kudumu jambo ambalo lilizua maswali mengi.
Alikimbia nchi hiyo baada kukwepa kulipa dhamana ya madai udanganyifu na utakatishaji fedha.
Waziri wa mambo ya ndani Aaron Motsoaledi alisema maofisa watano waliadhibiwa baada ya uchunguzi kumalizika.
Waziri alikanusha madai kuhusu idara ya mambo ya ndani na maofisa wake walimsaidia kurahisisha mambo ya mchungaji huyo.
Bwana Bushiri yupo Malawi na kesi yake bado haijaisha

No comments:
Post a Comment