Search This Blog

Thursday, September 9, 2021

Kenya yatangaza ukame kuwa janga la taifa

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametangaza kuwa ukame umeathiri baadhi ya sehemu za Kenya na hivyo ni janga la taifa.

Ukame huo umeathiri kaunti 10 kati ya kaunti 47 . Watu wapatao milioni mbili wameathirika nchini Kenya.

Rais ametaka wahanga wa janga hilo kusaidiwa na wizara ya mambo ya ndani.

Rais ametangaza hayo baada ya mkutano na viongozi wa eneo lililoathirika kaskazini mwa nchi hiyo, ambako hawajapata mvua kwa kiwango cha nusu ya 50%.

Wakazi wa eneo lililoathirika ,ambao ni wafugaji wanakabiliwa na njaa na wanyama wao wanakufa.

Serikali imesema itachukua hatua madhubuti kukabiliana na ukame huo.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...