Search This Blog

Sunday, September 12, 2021

Kalipina amjibu Wema kuhusu kupigwa

 


Msanii wa HipHop Kalapina Nabii Koko amemjibu Wema Sepetu kwa kusema kwamba mwanamke hapigwi bali kuna njia za kumfanyia kama ukiona mwanamke wako ana maneno sana.


Kalapina amejibu hilo baada ya ujumbe wa Wema Sepetu kusema mtu kupigwa na 'baby' wake kuna raha yake na yeye binafsi ana-enjoy kupigwa.


"Mwanamke hapigwi, ukiona mtu anampiga mwanamke huyo ni 'bushaman' kwa sababu wao ndio wana mambo hayo, mwanamke anapigwa kwa zawadi ukiona kelele nyingi we mpe zawadi tu" amesema Kalapina


Kalapina ameongeza kusema kwenye upande wa mahusiano yeye ni mwamba na anamjua Wema Sepetu labda amemaanisha kupigwa kwa aina nyingine.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...