Serikali ya Sudan inasema kumekuwa na jaribio la mapinduzi lililotibuka katika nchi hiyo na hatua zinachukuliwa kudhibiti hali hiyo, vyombo vya habari vya serikali vinaripoti.
"Kumekuwa na jaribio la mapinduzi lililoshindwa, watu wanapaswa kukabiliana nalo, "Shirika la habari la AFP linanukuu ripoti zikisema.
Kulikuwa na jaribio la kuchukua jengo ambalo lina vyombo vya habari vya serikali, Shirka la habari la AFP linasema likiashiria chanzo cha serikali.
Msemaji wa serikali amesema shughuli ya kuwahoji wanaoshukiwa kuwa nyuma ya jaribio hilo la mapinduzi itaanza muda mfupi ujao.

No comments:
Post a Comment