Search This Blog

Tuesday, September 7, 2021

DRC Yapokea dozi 250,000 za chanjo ya Moderna



Rais wa DRC, Felix Tshisekedi mwenyewe alisita kuchukua cha ya AZ na kuahidi kupewa chanjo tofauti wakati zitakapopatikana nchini.

Kundi hili la kwanza la dozi 250,000 za chanjo ya Moderna ni sehemu ya chanjo milioni sita tofauti ambazo Nchi hiyo ya Afrika ya Kati imekuwa ikingojea tangu, Julai iliyopita.

DRC ni moja ya nchi ambazo kuna pingamizi ya juu kupokea chanjo ya Corona barani.

Tangu kuzinduliwa kwa kampeni ya chanjo dhidi ya covid-19, mnamo Aprili 19, 2021, chini ya watu laki moja wamepokea chanjo hizo. Zaidi ya dozi elfu 300 za AZ zililazimika kuharibiwa wakati zilipomalizika muda wa matumizi Juni na Julai iliyopita

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...