Search This Blog

Sunday, September 5, 2021

Balozi wa Indonesia awaahidi mambo mazuri wachimbaji wadogo wa madini ya jasi wilayani Kilwa


Na Ahmad Mmow, Lindi.

Balozi wa Indonesia nchini Tanzania, Profesa Ratlan Pardede ameahidi kutafuta soko la madini ya aina ya jasi nchini Indonesia  ili kukabilianana changamoto ya kutokuwepo kwa masoko ya uhakika ya madini hayo.

Profesa Pardede alitoa ahadi hiyo jana katika kijiji cha Kiranjeranje, wilayani Kilwa alipotembelea eneo linalo tumika kupakia na kusafirisha jasi inayotoka migodini.


Profesa Pardede ambae aliahidi hio baada ya kusikia maelezo ya katibu wa wachimbaji wadogo wa jasi katika wilaya ya Kilwa, Elias Kabwebwe, alisema baada ya kusikia maelezo na changamoto zilizoelezwa atatafuta masoko ya madini hayo nchini Indonesia ili wachimbaji wanufaike na kazi wanayofanya.

Licha ya ahadi hiyo, pia  Profesa Pardede aliahidi atazungumza na kampuni zinazotengeneza bidhaa zinazotokanana jasi nchini Indonesia kuja kujenga viwanda  vinavyotengeneza bidhaa zinazotokanana madini hayo.

Awali katibu wa umoja wa wachimbaji wadogo wa jasi wilayani  Kilwa, Elias Kabwebwe alisema licha ya jasi inayopatikana wilayani humo kuwa bora kuliko inayopatikana katika nchi nyingine zote zilizopo barani Afrika, lakini miongoni mwa changamoto kubwa ni soko la uhakika.

Kabwebwe pia alisema litakuwa jambo jema iwapo kutajengwa viwanda vya kutengeneza  bidhaa zinazotokanana madini hayo wilayani Kilwa ili kuyaongezea thamani na kuzalisha ajira kwa wananchi. Huku akiitaja changamoto nyingine kuwa ni mitaji midogo. Hali inayosababisha watumie vifaa duni vya kuchimbia.

Licha ya kutembelea eneo hilo katika wilaya hiyo ya Kilwa, balozi  Profesa Pardede alitembelea vivutio vya utalii vya mambo ya kale katika eneo la Kilwa Kisiwani. Ambapo pia alifanya utalii wa baharini.

 



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...