Search This Blog

Sunday, August 8, 2021

Shambulizi la bomu nchini Afghanistan


 

Raia 12 waliuawa kwenye shambulizi la bomu lililotekelezwa katika mkoa wa Paktiya nchini Afghanistan.

Katika taarifa iliyotolewa na Idara ya Polisi ya Paktiya, iliripotiwa kuwa bomu lililonaswa barabarani katika kijiji cha Chinu cha wilaya ya Seyid Kerem mkoa huo kililipuliwa wakati gari lililokuwa limebeba raia lilikuwa likipita katika eneo hilo.

Ilielezwa kuwa raia 12, wakiwemo watoto, walipoteza maisha na raia 2 walijeruhiwa katika shambulizi hilo.

Idara ya Polisi ililaumu Taliban kwa kuhusika na shambulizi hilo.

Mpaka sasa bado hakuna mtu yeyote aliyedai kuhusika na shambulizi hilo.



No comments:

Post a Comment

Punguza kilo tano kwa siku saba

  NI watu wachache wanaopenda kunenepa, wengi wanapenda miili ya wastani kwa kuwa  unene si mzuri. Ukiwa mnene si tu kwamba unakaribisha m...